• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO AKILI KUTORIDHISHWA NA KASI YA UJENZI WA STENDI MPYA YA DALA DALA

Posted on: November 23rd, 2019

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, amesema kasi ya ujenzi wa Stendi Mpya ya Dala Dala hairidhishi, hivyo ametoa wito kwa Mkandarasi wa mradi huo kuongeza kasi ili mradi uweze kukabidhiwa kwa Wananchi kwa muda uliopangwa.

Akizungumza wakati wa ziara ya kutembelea mradi huo leo Novemba 23, amesema bado mradi huo unashida kwani idadi ya wafanyakazi waliopo ni wachache  ukilinganisha na ukubwa wa eneo na kazi zinazotakiwa kufanyika.

Aidha, amesema kuwa ifikapo tarehe 31 Desemba, 2019 pesa iliyotolewa na wafadhili kwaajili ya mradi huo itachukuliwa na wafadhili kwakuwa mda wa mradi utakuwa umeisha hivyo kuna haja ya kuhakikisha kazi inafanyika usiku na mchana ili pesa hiyo isiondoke na mradi ukamilike kwa wakati.

"Mkandarasi  kwakweli sijaridhishwa na kasi ya ujenzi, pia huwezi kuwa na mradi mkubwa kama huu harafu ukawa na wafanyakazi wachache unafikiri kweli kwa muda tulio nao tutaweza kukamilisha kwa wakati? niwaombe ongezeni vibarua muda umekwisha hii asilimia 40% ya ujenzi wa Stendi mliyoniambia sijaridhika nayo, nataka nikija nikute kazi zimefanyika kwa kiwango kikubwa, tambueni pesa za mradi huu zina masharti mwezi Desemba ujenzi uwe umekamilika ili wananchi waweze kupata huduma,haiwezekani Mhe. Rais  Dkt John Magufuli aje kufungua mradi akutane na mabango"Amesema DC Chonjo.

Amemtaka Mkandarasi, mshauri wa mradi pamoja na Mhandisi wa Manispaa kukaa pamoja katika vikao vyao ili kuweza  kuangalia  vipaumbele vya ujenzi, kwani kitu cha kwanza kilichotakiwa kujengwa ni Stendi na sio jengo la utawala.

Amesema kitu muhimu kilichohitajika katika ujenzi wa Jengo la utawala ilikuwa ni Choo, miundombinu ya maji pamoja na umeme lakini sio jengo la utawala ambalo litakuwa na watu wachache kuliko Stendi ya Daladala.

Aidha  DC Chonjo amesema Bilioni 5.2,  mkandarasi alizochukua kwaajili ya ujenzi wa stendi hiyo, mradi huo ulipaswa uwe na huduma zote kama zilizopo kwenye Stendi ya zamani kwani haitakuwa jambo rahisi kuwaambia Wananchi wahamie Stendi mpya harafu huduma muhimu zinakosekana itakuwa ni jambo baya na litaleta mtafaruku kwa Wananchi.

Amesema anataka kuona Stendi hiyo ikiwa na maeneo ya Vioski , maeneo ya Wajasiriamali wadogo wadogo wamamchinga, wauza urembo pamoja na Mama lishe na Baba lishe, hivyo kama vitu hivyo vitakosekana itakuwa haina maana ya kuwepo na mradi mkubwa kama huo.

DC Chonjo amewaagiza Wahandisi wa TARURA, Mshauri wa mradi pamoja na mhandisi wa Manispaa kukaa kwa pamoja waone ni namna gani mradi huo utakavyo pokelewa kwa Wananchi.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amesema kasi ya ujenzi ipo chini hivyo amemtaka mkandarasi kuongeza vibarua kama Mkuu wa Wilaya alivyoshauri ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Amesema ingependeza zaidi  kama wangeanza na ujenzi wa vibanda vya maduka vya wafanya biashara kuliko kuendelea kuweka nguvu katika ujenzi wa jengo la Utawala ambalo sio kipaumbele katika mradi huo.

"Hapa mshakosea lakini niwaombe bado muda mnao hakikisheni mnaweka nguvu katika ujenzi wa Stendi ili hawa wananchi waweze kutumia kwani jengo la utawala lilikuwa halina umuhimu kwa sasa zaidi ya Stendi, ongezeni kasi tunachotaka sisi ni kuona matokeo ili hii pesa tuliyopewa kwa masharti tunufaike nayo kabla haijachukuliwa, ikichukuliwa mradi tunaukosa na nyie pia hamtapata pesa" Amesema Mhe. Kihanga.

Naye Mshauri wa Mradi , Mhandisi. Antonio Mkinga, amesema mradi huo ulitakiwa kumalizika Mei 25, 2020 lakini kati kati ya Mwezi Oktoba, 2019 kulitolewa agizo la kutaka mradi ukamilike ifikapo Desemba 31, 2019.

Amesema walishamwandikia barua mkandarasi wa mradi ya kumuelekeza kuongeza vibarua lakini cha kushangaza hadi sasa bado vibarua hao hawajaongezwa.

Aidha , amemtaka Mkandarasi wa mradi kuongeza mashine pamoja na vifaa kwenye eneo la mradi ili kasi ya ujenzi iende na kukamilisha mradi kwa wakati na kuweza kutoa huduma kwa wananchi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa