• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO ASAKA MWAROBAINI KWA MADIWANI HUJUMA ZA MIUMDOMBINU YA TANESCO MORO

Posted on: May 23rd, 2018

MKUU wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo amewaagiza watendaji wa mitaa na kata katika Manispaa ya Morogoro kushirikiana na madiwani kuhakikisha miundombinu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) inakuwa salama dhidi ya hujuma mbalimbali katika maeneo yao.

Mkuu huyo wa wilaya alitoa agizo hilo katika kikao cha pamoja kati ya madiwani , watendaji wa kata, viongozi wa halmashauri ya Manispaa na wa Tanesco mkoa wa Morogoro katika kikao kilichofanyika  kwa ajili ya kujadili namna ya kudhibiti hujuma za miundombinu ya shirika hilo.

Alisema , Shirika la Tanesco mkoa wa Morogoro limekuwa likikabiliwa na changamoto ya kuhujumiwa kwa miundombinu yake zinazofanywa na watu wasiojulikana na kurudisha nyuma jitihada za shirika hilo za kuwaletea maendeleo wananchi.

Katika kusaka suhuhu hiyo aliutaka uongozi wa Tanesco mkoa kusaidia kupata orodha ya watumishi waliokuwa wameondolewa kwenye ajira ikiwa ni kwa kustaafu, watumishi hewa , vyeti vya kugushi na wengineo na orodha hiyo iwasilishwe Kituo kikuu cha Polisi kwa ajli ya ufuatiliaji wa karibu juu ya nyendo zao.

Hata hivyo alisema, ili kukabiliana na hujuma hizo, Serikali ya wilaya ya Morogoro imeamua kupiga mafurufu shughuli za kibinadamu kando kando na miundombinu ya Tanesco , kuzuia misumeno ya moto ikiwa ni pamoja na Tanesco kuongeza suala la utoaji wa elimu kwa wananchi .

Kwa upande wake , Meneja wa Tanesco mkoa wa Morogoro Mhandisi Hassan Said katika taarifa yake katika kikao hicho alisema , katika kipindi cha miaka miwili na nusu zaidi matukio 22 ya kuhujumiwa kwa miundombinu ya Tanesco yamejitokea ikiwemo ukataji wa nguzo za umeme, wizi wa nyaya, na uharibifu wa transfoma.

“ Mwaka 2016 pekee kulikuwa na matukio nane ya kuhujumiwa kwa miundombinu ya Tanesco ndani ya Manispaa ya Morogoro ,mwaka 2017 matukio manne na kwa mwaka huu hadi kufikia mwezi Mei ni matukio sita jambo hili hata mwaka haujamalizika , na kibaya zaidi licha ya juhudi za kushirikiana na vyombo vya dola hakuna mtu aliyekamatwa " alisema Mhandisi Said.

Nao baadhi ya wajumbe wa kikao hicho ambao wengi wao walikuwa ni madiwani kwa nyakati tofauti walitoa ushauri kwa Tanesco kwa kuitaka kuboresha mahusiano na jamii, kuzifanyia kazi haraka kero za wateja wao ikiwa na kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa wanapokuwa katika majukumu yao ya kazi .

Diwani wa Kata ya Boma , Amir Nondo alisema , ni vyema wafanyakazi wa Tanesco wanapokuwa na majukumu yao mitaani wapitie ofisi za mitaa kutoa taarifa ili wananchi watambue uwepo wao kwani bila kufanya hivyo waaarifu nao wanatumia mwanya huo kujipenyeza kuharibu miundombinu ya shirika .

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa