• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC CHONJO AWATAKA WENYEVITI WA MITAA MANISPAA MOROGORO KUZINGATIA MAADILI KATIKA UTENDAJI WAO WA KAZI

Posted on: January 7th, 2020


MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, amewataka Wenyeviti wa Serikali za Mitaa Manispaa ya Morogoro, kuchapa kazi kwa kufuata katiba ya Nchi na Miongozo ya kiutendaji ya Serikali za Mitaa na maadili ikiwa ni pamoja na kushirikiana na Watendaji wa Serikali katika maeneo yao ya kazi ili kuwaletea Wananchi maendeleo na kutatua kero zao kwa wakati.

Akizungumza na Waandishi wa habari leo Januari 7, 2020, katika Semina elekezi ya mafunzo kwa Wenyeviti wa Mitaa, iliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Manispaa , amesema kuwa ili maendeleo yaje kwa haraka lazima wenyeviti na watendaji wawe kitu kimoja na kuzingatia misingi ya Uongozi ya Utawala bora.

Amesema Wenyeviti wa Mitaa hawana tofauti na Viongozi wowote wanaosimamiwa na Serikali katika ngazi za Wilaya, Mkoa na Taifa, hivyo kila mmoja wao afuate misingi ya Uongozi katika kutoa huduma kwa Wananchi.

"Nisingependa kusikia Mwenyekiti wa Mtaa anauza Ardhi za Wananchi, anadhulumu mashamba ya wananchi, mimi ni msimamizi mkuu wa Serikali katika Wilaya sitalifumbia macho suala hilo, ifahamike kuwa kumekuwepo na tabia ya wenyeviti wa Mitaa wasio waadilifu katika pesa pale wananchi wanapofika kwao kuhitaji huduma fulani, wenyeviti mnapaswa kuwa wazalendo na kuishi kwa kuwa waadilifu na wachapa kazi kwa wananchi waliowachagua" Amesema DC Chonjo.

Amewataka Wenyeviti wa Mitaa na Wajumbe wao kufanya kazi kwa uadilifu na uzalendo katika kuwatumikia wananchi ili kuendana na kasi ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli ya kuwaletea maendeleo wananchi.

Hata hivyo alichukua nafasi ya kuwapongeza wenyeviti hao kwa kuchaguliwa na kuwaeleza kuwa  ushindi wao haikuwa kazi rahisi hivyo amewataka wafanye kazi kwa bidii ili wasikiangushe chama kilichowaweka madarakani.

Amesema imani yake ni kwamba baada ya mafunzo hayo wenyeviti wa mitaa watakuwa tayari kufanya kazi kwa mujibu wa Sheria, kanuni, Taratibu na miongozo mbalimbali inayotolewa na Mamlaka na kupunguza migogoro pamoja na malalamiko  yanayojitokeza yanayopelekea wananchi kuyafikisha kwa Mkurugenzi, Mkuu wa Wilaya au Mkoani.

" Naimani pia mtaboresha mahusiano mazuri na watendaji wenu wa Mitaa na Kata na mtaenda kutekeleza shughuli zenu kwa ushirikiano wa karibu , hakikisheni mnazingatia misingi ya Utawala bora katika utendaji wenu wa kazi bila upendeleo wa aina yoyote wa kisiasa, kidini na kikabila na mumtangulize Mwenyezi Mungu kwa kila jambo" Ameongeza DC Chonjo.

"Wenyeviti wa Mitaa nyie ni wawakilishi katika Jamii na hamna budi kuwashirikisha wale mnaowaongoza ili kwa pamoja kupiga hatua ya kushinda maadui wa Taifa yaani Umasikini, Ujinga , Maradhi na pia rushwa ambayo sasa ndiye adui wa haki na anachangia katika kudhoofisha vita dhidi ya wale maadui wetu wale watatu wa awali" Ameongeza  DC Chonjo.

Pia Mkuu wa Wilaya huyo, amesema hali ya usafi katika Mitaa bado hairidhishi, amewataka wenyeviti wasimamie kikamilifu vikundi vya uzoaji taka na kufuata sheria ya usafi ili kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na wale watakao kiuka sheria wafikishwe kwake na kuchukuliwa hatua za kisheria.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amemshukuru na kumpongeza DC Chonjo kwa kufungua mafunzo hayo, huku akisema ili kutekeleza dhana ya Uongozi unaolenga kumletea mwananchi maendeleo endelevu, wenyeviti wa mitaa wanapaswa kuzingatia maadili ya uongozi na pia misingi ya Utawala bora ikiwamo kutenda haki kwa kuzingatia Utawala wa Sheria na kutimiza wajibu wao kikamilifu.

" Naimani mafunzo haya yatawasaidia kuboresha  mahusiano mazuri na watendaji wenu wa Mitaa na Kata na mtaenda kutekeleza shughuli zenu kwa ushirikiano wa karibu , hakikisheni manazingatia misingi ya Utawala bora katika utendaji wenu wa kazi bila upendeleo wa aina yoyote wa kisiasa, kidini na kikabila na mumtangulize Mwenyezi Mungu kwa kila jambo" Ameongeza Sheilla .

Naye Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amesema kama wenyeviti hawatakuwa na maadili basi hata maendeleo kwenye mitaa yao watayasikia kwenye bomba hivyo amewataka wenyeviti kuhakikisha wanatunza na kusimamia vyema miradi iliyo katika maeneo yao ili iweze kuwanufaisha wananchi  na kuleta maendeleo katika mitaa yao.

Hata hivyo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Morogoro, Fikiri Juma, amewataka wenyeviti wa Mitaa wasiwe kero kwa wananchi badala yake wawe mfano bora wa kuhakikisha maendeleo kwa wananchi yanapatikana kwa haraka.

"Nyie ni wenyeviti mmepewa mamlaka makubwa katika mitaa yenu , tumieni ushawishi  na mamlaka mliyonayo kuhakikisha mnawatunzia siri za faragha wale mnaowaongoza, hiyo ndiyo sifa ya kiongozi, mtaa mchafu wewe upo, maji hakuna wewe upo matukio ya ukatili yanatokea wewe upo, badilikeni msifanye kazi kwa mazoea tunataka matokeo chanya wananchi waliwaamini wakawapatia ridhaa itumieni hiyo nafasi vizuri tumsadie Mhe. Rais katika kuwaletea maendeleo wananchi" amesema Fikiri

Afisa TAKUKURU Mkoa wa Morogoro, Fredrick salwa, amewataka wenyeviti kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizopo huku akiwataka wananchi kutoa ushirikiano na TAKUKURU .

"Mihuri mliyopewa siyo ya kujinufaisha, toeni taarifa ya vitendo vya rushwa , mwananchi anatarajia kuona ukipambana na vitendo vya rushwa, morogoro bila vitendo vya rushwa inawezekana' Amesema Fredrick.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa