• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MOROGORO NA MKURUGENZI MANISPAA WATOA MSAADA WA MAHITAJI KITUO CHA WATOTO YATIMA MGOLOLE NA TV KITUO CHA WAZEE FUNGAFUNGA.

Posted on: January 1st, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro , Sheilla Lukuba wametembelea kituo cha watoto yatima cha Mgolole na kambi ya wazee ya Fungafunga na kutoa mahitaji ya watoto na TV aina ya Samsung katika kituo cha wazee.

Akikabidhi vitu hivyo vyenye thamani ya Tsh 1,008,000.00 katika kituo cha watoto yatima Mgolole Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, amesema kuwa Ofisi yake na Manispaa kwa ujumla iko pamoja nao na itaendelea kushirikiana nao kwa mazuri na changamoto yeyote itakayojitokeza katika makazi ya watoto hao, hivyo wasisite  kutoa taarifa pale wanapokuwa na tatizo lolote.

“Nimefurahishwa sana na huduma mnazowapatia watoto wetu, kwakweli mnastahili pongezi kubwa, ni wachache wenye moyo kama wenu wa kuwasaidia hawa watoto, msikate tamaa endeleeni na malezi bora mwenyezi mungu atawabariki sana chukueni hiki kidogo tulichowaletea ikiwa ni sehemu yetu ya kusherekea mwaka mpya na watoto wetu wajisikie huru na amani badala ya kuwa wapweke”Amesema DC Chonjo.

Pia amempongeza mlezi wa kituo hicho, Sister Palagia Maria, kwa kuwa na malezi mazuri kwa watoto hao wanaoletwa kwenye makazi hayo  kutoka katika mazingira hatarishi.

Aidha Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema kuwa huo ni mwendelezo wa ahadi zilizotolewa na Mkuu wa Wilaya kwa kushirikiana vyema na Uongozi wa Manispaa ya Morogoro huku akisema kuwa  tayari baadhi ya ahadi zimekwisha tekelezwa na zawadi nyingine kutoka kwa wahisani hivyo amemtaka mlezi wa makazi hayo kuendelea na moyo wa kuwasaidia  watoto hao hadi pale watakapo pata mwanga wa maisha yao.

“Watoto niwaombe msome sana mkizingatia hakuna urithi zaidi ya elimu, Serikali ya awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli imeweka mpango wa elimu bila malipo msome sana ili nanyi baadae muweze kuwa na maisha mazuri na kuendesha familia zenu” Amesema Sheilla.

Naye, Mlezi wa makazi hayo, Sister Palagia Maria, amemshukuru Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi ikiwamo Ustawi wa Jamii kwa kuwa karibu nao huku akiwataka wasikate tamaa kwani wao wanategemea pia misaada kutoka kwa wahisani.

Mbali na kutoa chakula pamoja na Vinywaji katika Makazi ya Mgolole, Mkurugenzi Sheilla amepata nafasi ya kutembele kituo cha kulelea Wazee wasiojiweza cha Funga Funga kilichopo  Manispaa ya Morogoro na kutoa zawadi ya TV Flat Screen na king’amuzi cha Star Times vyenye thamani ya Tsh 670,000.00.

Amesema lengo la kutoa Tv hiyo ni kuwafanya Wazee hao waweze kuangalia taarifa  mbali mbali za miradi ya maendeleo inayotekelezwa  na Serikali ya Awamu ya tano chini ya Mhe. Rais Dkt. John Magufuli.

Kwa upande wake Afisa Mfawidhi Kituo cha Funga Funga, Bi Yolanda Komba,amemshukuru Mkurugenzi na Idara ya Ustawi wa Jamii kwa kuwa karibu na kuwasaidia katika huduma mbali mbali ikiwamo kuwapatia msaada na kuwajali wazee  hao wenye mahitaji muhimu hivyo anamtakia kazi njema katika kutekeleza majukumu yake na kuanza mwaka mpya kwa mafanikio zaidi.

Naye Mwenyekiti wa Wazee hao, Mzee Joseph Kaniki, ameushukuru Uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kutekeleza kile walichokiomba huku akizidi kumuombea Mhe. Rais Magufuli afya njema ili aweze kuiongoza vyema Tanzania katika kufikia maendeleo hususani uchumi wa Kati na wa Viwanda.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa