• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA ATAKA HUDUMA ZA AFYA KITUO CHA UHURU (NUNGE ) KUBORESHWA

Posted on: November 12th, 2020

MKUU wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kuboresha huduma za afya katika Kituo cha afya cha Uhuru (Nunge), kufuatia kituo hicho kuzidiwa na Wagonjwa.

Kauli hiyo ameitoa Novemba 12 wakati wa ziara ya kukagua na kuzungumza na Uongozi wa Kituo cha afya cha Uhuru (Nunge) kufuatia kituo hicho kuzidiwa na Wagonjwa na ufinyu wa eneo.

“Tumejionea hali ilivyo, tumegundua wagonjwa wanaofika hapa wanafikia 280 hadi 300 sasa idadi hii ni kubwa sana, kwahiyo tumekubaliana na Manispaa tujenge Ghorofa pamoja na kuongeza idadi ya madaktari , watumishi na wauguzi, lakini pia tumefikiria kuwe na utaratibu katika vituo vyetu vya afya wawe wanabadilishana wataalamu wanapoona kuna sehemu inapwaya ili kuwe na huduma ambayo haitasubiria maelekezo kutoka ngazi za juu, hili litasaidia sana kutoa huduma bora kwa wagonjwa wetu” Amesema DC Msulwa.

Katika hatua nyengine, amesema watawasiliana na Wizara ya afya kupitia Bohari ya dawa waongeze dawa za kutosha ili kuweza kumudu huduma zinazotolewa.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, ameahidi kukarabati Kituo cha Afya cha Uhuru (Nunge) kuwa ghorofa ili kupunguza adha ya Wagonjwa katika Kituo hicho.

Lukuba, amesema katika kipindi hiki ambacho anatafakari jinsi ya kufanya ukarabati huo , ameandaa eneo la Karibu na Mango Garden ambalo litatumika kwa ajili ya kutolea huduma ya mama na mtoto.

“Mkuu wa Wilaya ametoa ushauri, tumeupokea , na tunaangalia eneo la wazi ambapo tunatarajia kutenga eneo la Mango Garden kwa ajili ya kuhamisha huduma za Mama na Mtoto kuhamia huko ili kupisha huduma nyengine ziendelee, lakini tutakarabati hapa kwa kujenga Ghorofa ili tuzidi kuimarisha huduma za afya kutokana na idadi kubwa ya Wagonjwa wanaokuja hapa kupata huduma” Amesema Lukuba.

Aidha, amewataka Madaktari na wauguzi wafanye kazi kwa bidii ikiwamo kutumia lugha nzuri kwa wateja wao kwani wagonjwa wanapokwenda kupata huduma wanahitaji lugha nzuri ili waweze kupata faraja.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa