• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC MSULWA AZINDUA STENDI YA KALOLENI MANISPAA YA MOROGORO HUKU AKIWATAKA WANANCHI KUITUNZA MIUNDOMBINU ILIYOPO

Posted on: November 6th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Bakari Msulwa, amezindua stendi ya daladala Kaloleni na kuwataka wananchi kutunza miundombinu iliyopo  kwa sababu ujenzi unatokana na kodi.

Kauli hiyo ameitoa leo Novemba 06/2020, wakati wa uzinduzi wa Stendi ya Daladala ya Kaloleni iliyopo Kata ya Mji Mpya Manispaa ya Morogoro.

Msulwa, amesema kuwa licha ya kuwa haki yao, njia moja wapo ya kuthamini fedha zao ni kulinda miundombinu iliyopo na inayoendelea kujengwa.

“Tatizo kubwa tulilo nalo ni kushindwa kutambua haki na wajibu wetu kama walaji, hiyo ndiyo sababu inayotufanya kugharamia vitu ambavyo kama tungevitunza vizuri tusingetarajia kupata gharama hizo, kwahiyo ni wajibu wetu kuthamini fedha zetu maana zinatokana na kodi zetu wenyewe" Ameongeza  kusema DC Msulwa.

“Manispaa ya Morogoro ni Mji Kongwe sana , kwa hili lililofanyika leo naupongeza sana Uongozi wa Manispaa ya Morogoro kwa kuonesha na kuufanya Mji huu kuwa sura ya Manispaa, lakini niseme unapokuwa na Uongozi mzuri ngazi ya Kitaifa, Jimbo na Kata unatengeneza uelekeo mzuri wa kutengeneza maendeleo kwa wananchi au taasisi husika, kwahiyo uchaguzi umekwisha, matokeo tumeyasikia na Viongozi wetu wameshaanza kufanya kazi lakini tunasubiria waapishwe ili waweze kujipanga vizuri ” Amesema Msulwa.

Aidha, amesema lengo la Manispaa hii ni kuwa Jiji hivyo ni lazima miundombinu iweze kuboreshwa licha ya kuwa zipo changamoto zitakazojitokeza.

“Hatuwezi kukaa katika Manispaa kwa miaka 32 na tukaendelea kukaa kwa muda mrefu kabla ya hatujafika kiwango cha kuwa Jiji, lakini ukishakuwa Jiji lazima utarajie changamoto mbalimbali, changamoto hizo pia zinaweza kugeuka kuwa fursa , kwahiyo hatua ambazo Manispaa imezichukua zinatufanya kuelekea kuwa Jiji, nafahamu ukiachia stendi hii ya Kaloleni, kuna Stendi kuu ya Daladala Mafiga, Soko Kuu la Kisasa, na miradi mingine ambayo inaendelea nawapongeza sana Manispaa, Wahandisi wa miradi kwa kazi kubwa na nzuri mnazo fanya,””Ameongeza DC Msulwa.

Pamoja na hayo amesema ni vizuri pia Mkurugenzi wa Morogoro Vijijini kufika hapa na timu yake ya Uongozi ili nao waweze kujifunza na wao wakajenge Stendi kama hii kwa ajili ya kurahisisha huduma za usafiri kwa Wananchi wao.

Mwisho , DC Msulwa, ameahidi kiasi cha Shilingi Milioni Moja kwa ajili ya ukarabati wa Kituo kidogo cha Polisi cha Mji Mpya.

Naye Kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Michael Waluse, mbali na kushukuru kwa pongezi zilizotolewa katika ofisi yake, ameahidi kushirikiana na Uongozi wa Daladala wa Stendi hiyo kwa yale yote yatakayojitokeza kuhusiana na Stendi hiyo.

Waluse, amesema kuhusu Ukarabati wa Kituo kidogo cha Polisi kilichopo jirani na Stendi hiyo, katika vikao swala hilo litajadiliwa na kuona ni jinsi gani Manispaa itakavyoweza kushiriki katika hatua hiyo ya ukarabati ili iendane na hadhi ya Stendi hiyo kwani Jeshi la Polisi ndio watu wa kwanza katika kulinda amani katika eneo hilo.

Kwa upande wa Msimamizi wa fedha za mkopo wa Benki ya Dunia chini ya fedha za uboreshaji Miji ( Urban Local Government Strengthening Program (ULGSP) na Mhandisi wa TARURA Manispaa ya Morogoro, James Mnene, amesema mradi huo umegharimu kiasi cha Shilingi milioni 644 ambapo ujenzi wake ulianza Aprili 28/2020.

Mnene, amesema mkandarasi Nandhra amekamilisha Ujenzi huo kwa asilimia mia moja kama ilivyoonekana wakati wa ukaguzi kabla ya kuzinduliwa.

“Mradi umekamilika kwa asilimia mia moja kama mnavyoona,lakini kazi ambayo imebakia ni kuweka alama za kuongoza magari lakini kazi hizi zote zitafanyika katika kipindi cha matazamio,mpaka sasa Mkandarasi ameshalipwa shilingi milioni 566 sawa na asilimia 74.9 na kiasi kilichobakia atalipwa baada ya kuwasilisha madai yake ya mwishoni na matumaini ya Manispaa ya Morogoro katika Stendi hii ya Daladala ni kutoa huduma bora ya usafiri kwa magari ya Daladala yapatao 50 na kuongeza Manispaa mapato na hadi sasa hakuna kipingamizi chcochote cha kutofanya stendi hii kutotumika “ Amesema Mnene.

Hata hivyo, Diwani mteule wa Kata ya Mji Mpya, Emmy Kiula, amemshukuru Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Mhe. Bakari Msulwa , kwa kukubali ombi lake la kukarabati Kituo kidogo cha Polisi cha Kata ya Mji Mpya kufuatia Mkuu wa Wilaya kuahidi kiasi cha Shilingi Milioni moja.

Mwenyekiti wa Umoja wa Madereva wa Daladala Mkoa wa Morogoro, Hemed Ntengwa, amesema Stendi hiyo ilikuwa changamoto sana lakini kwa sasa watafanya kazi vizuri na kuitunza miundombinu ya Stendi hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa