• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

JAFO AFURAHISHWA NA UJENZI WA SOKO KUU LA MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: August 14th, 2020

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa TAMISEMI Mhe. Selemani Jaffo ameonyesha kufurahishwa na ujenzi wa soko kuu la kisasa katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro katika ujenzi ambao umekamilika kwa asilimia 99 ambapo umegharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 17.6

Akizungumza mara baada ya kutembelea na kuona maeneo mbalimbali katika soko hilo Mhe. Jaffo amesema kuwa licha ya kuwepo na ujenzi wa miradi ya masoko katika Mikoa ya Mtwara, Dodoma, Njombe na Dar es Salaam ujenzi wa soko la Kisasa Manispaa ya Morogoro ni wa kipekee na wenye viwango vya hali ya juu kutokana na ujenzi huo kuwa umezingatia mahitaji ya wafanyabiasha wanataka nini katika soko hilo.

“Mimi huwa nakuja kukagua kazi sio kutembelea na nimefika mara nyingi katika soko hili,awali nilikuwa siridhishwi na kasi ya ujenzi ila leo binafsi nimefurahishwa sana baada ya kufika hapa na kuona jinsi wakandarasi wetu wazawa walivyoweza kujenga kwa ubora unaoridhisha. Hiki ni kitega uchumi kikubwa sana kwa Halmashauri na kitabadili mandhari ya Manispaa hii,kwa aliyefika hapa miaka mitano iliyopita leo hii akija anaweza kupotea hii ni heshima kubwa sana aliyotupatia Mhe.Rais Dkt John P.Magufuli kwa kuamua kutupa fedha za mradi mkubwa kama huu.”Alisema Jaffo.

"Nampongeza sana Mhandisi aliyesimamia ujenzi huu,pia nawapongeza viongozi na watumishi wote wa Manispaa ya Morogoro kwa ushirikiano mliouonyesha katika utekelezaji wa mradi huu ,hii inaonyesha jinsi gani mlivyo makini katika usimamizi wa miradi,Manispaa ya leo siyo jana angalia sasa mna stendi ya Msamvu,mmejenga stendi ya daladala,haya ni mafanikio makubwa sana katika Serikali ya awamu ya tano"Aliongeza  Mhe.Jaffo.

Aidha Mhe. Jafo ameahidi kushughulikia changamoto ya msamaha wa ongezeko la thamani VAT na kuhahidi kuifikisha katika mamlaka husika kwa kuwa miradi inayofadhiliwa na Benki ya Dunia haitakiwi kutozwa kodi.

 “Lengo la miradi hii ni kwa ajili ya kukuza Miji na kuzijengea Halmashauri uwezo wa kujitegemea swala la msamaha wa VAT ni changamoto inayoikabili miradi mingi inayosimamiwa na TAMISEMI na hapa naona tena changamoto hii inajirudia licha ya Mheshimiwa Rais kutoa maelekezo kuhusiana na suala hili. Naomba nichukue changamoto hii na nitaiwasilisha kwa Waziri wa Fedha kwa utekelezaji."Alieleza Mhe.Jaffo.

 

Mradi wa soko kuu  unatarajiwa kuingizia Halmashauri mapato ya zaidi ya  shilingi Bilioni 2.3 kwa mwaka na hii itapunguza kutegemea ruzuku kutoka Serikali kuu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa