• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

KAMATI YA FEDHA HALMASHAURI YA WILAYA GEITA YAFANYA ZIARA YA MAFUNZO MANISPAA YA MOROGORO.

Posted on: April 22nd, 2019

Kamati ya fedha ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita akiwemo Mbunge wa jimbo la Geita Joseph Kasheku maarufu kama msukuma na mkuu wa Wilaya ya Geita Josephat Maganga wameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kubuni na kusimamia miradi mikubwa ya kimkakati ambayo itasaidia kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

Pongezi hizo walizitoa baada ya kamati hiyo kufanya ziara ya kimafunzo ambapo walitembelea  mradi wa ujenzi wa soko kuu la kisasa lililogharimu sh bilioni 17.6 na kituo cha mabasi cha msamvu kilichogharimu Sh.14 bilioni.

Akizunguimza katika majumuisho ya ziara hiyo Msukuma alisema kuwa pamoja na Halmashauri ya Wilaya Geita kuwa na mgodi mkubwa wa dhahabu lakini bado haijafanikiwa kujenga soko kubwa la kisasa na hata kituo cha mabasi cha kisasa hivyo ziara hiyo imewasaidia kujifunza mengi ikiwa ni pamoja na namna ya kubuni na kusimamia miradi mikubwa.

“Hii ziara imetusaidia kujifunza, tutakaporejea Geita tutaanza mchakamchaka wa kuanza kujenga soko kubwa kwa sababu uwezo tunao na hata eneo la kujenga tunalo,” alisema Msukuma.

Aidha aliiomba Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuwa tayari kuwapa wataalamu wa kuandika miradi mbalimbali kwa kuwa wamebaini Halmashauri hii inawataalamu wazuri na wenye ujuzi wa kutosha.

Hata hivyo Msukuma aliishauri Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kuongeza vyanzo vya mapato katika kituo cha mabasi cha msamvu badala ya kutegemea chanzo kikubwa kimoja cha ushuru wa mabasi ambao kwa sasa uko kwenye mchakato wa kufanyiwa marekebisho ya kisheria baada ya kuonekana kuwa ni kero kwa wamiliki wa mabasi.

Katika ziara hiyo Mkuu huyo wa Wilaya ya Geita Josephat Maganga alisema kuwa katika ziara hiyo amejifunza namna viongozi wa Manispaa ya Morogoro walivyokuwa naumoja na wanavyoweza kutekeleza na kusimamia miradi kwa kushirikiana.

Alisema kuwa kama viongozi wa Halmashauri wangekuwa hawaelewani isingewezekana miradi hiyo kutekelezwa kwa kiwango na kwa wakati bila kuathiri wananchi.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Morogoro Pascal Kihanga alisema kuwa ujenzi wa soko hilo ulikuwa na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaondoa wafanyabiashara waliokuwa wakifanya biashara kwenye soko la zamani.

Hata hivyo Kihanga alisema kuwa kutokana na viongozi wa Halmashauri  kuwa na msimamo, ushirikiano walifanikiwa kuwahamisha wafanyabishara hao bila vurugu hata hivyo baada ya kukamilika wafanyabishara hao watapewa kipaumbele kwa kuwapatia vizimba vya kufanyia biashara kwa gharama nafuu itakayopangwa na Halmashauri.

Awali akitoa taarifa za miradi hiyo Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro Michael Waluse alisema kuwa makusanyo ya mapato katika kituo cha mabasi msamvu kwa siku sio chini ya 3 milioni hata hivyo gharama za uendeshaji ikiwemo kulipa maji, umeme, usafi na misharaha ya watumishi wanaosimamia kituo hicho kwa mwezi sio chini ya Sh 25 milioni.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa