• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAPITIO YA MPANGO WA BAJETI NA MPANGO WA BAJETI WA MANISPAA YAWASILISHWA KWA BARAZA LA WAFANYAKAZI MOROGOR

Posted on: February 9th, 2024

Wasilisho la mapitio ya Mpango wa Bajeti wa Manispaa ya Morogoro kwa mwaka wa fedha 2022/2023, 2023/2024, na Mpango wa Bajeti wa Mwaka 2024/2025 kwa Baraza la Wafanyakazi, limefanyika tarehe 08.02.2024 kwenye ukumbi wa mikutano wa Manispaa hiyo na kuhudhuriwa na watu mbalimbali wakiwemo wawakilishi wa Divisheni na Vitengo vya Manispaa, na wawakilishi na viongozi wa vyama vya wafanyakazi ngazi ya mkoa.

Mwenyekiti wa kikao hicho, ndugu Jeremiah Lubeleje, akimwakilisha Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, wakati wa ufunguzi wa kikao amesema, dhima ya kikao hicho ni kuangalia mtazamo wa bajeti katika kuhakikisha inawaletea manufaa wananchi wa Morogoro hivyo wajumbe watumie fursa hiyo kuonesha wajibu wao na kutoa ushauri utakoleta tija zaidi.

Katika hatua nyingine, ndugu Lubeleje amesema makisio ya mapato ya ndani ya manispaa kwa mwaka wa fedha 2024/2025 yamepanda kwa asilimia 18.49 kwani katika bajeti inayoendelea hivi sasa makisio yalikuwa ni shilingi 13,185,280,000.00, na bajeti ya mwaka 2024/2025 makisio ni shilingi 15,622,877,022.05, shilingi 2,568,322,491.05 zikiwa ni mapato lindwa na shilingi 13,054,554,531.00 zikiwa ni mapato yasiyolindwa.

Ndugu Lubeleje ametaja miradi kipaumbele ya kimkakati ya Manispaa, ya mwaka 2024/2025 kuwa ni ujenzi wa maghala manne na eneo la kuegeshea malori katika eneo la SGR kata ya Kihonda.

“Miradi mingine ya kimkakati ambayo Manispaa inapanga kuitekeleza katika mwaka wa fedha 2024/2025 ni ujenzi wa ukumbi wa mikutano/sherehe na michezo ya watoto katika eneo la Manzese, ukumbi mkubwa, Hoteli ya nyota tano na nyumba maalum za kupangisha kata Mwembesongo, ujenzi wa kituo cha maegesho ya malori Nanenane kata ya Kichangani.

“Mingine ni ujenzi wa jengo la machinga kata ya Tungi, ujenzi wa shopping mall ya kisasa na Hoteli Msamvu kata ya Mafisa, ujenzi wa eneo la mapumziko na burudani kata ya Kihonda, ujenzi wa kituo cha michezo cha Uluguru, ujenzi wa Hoteli ya kisasa Kihonda mlimani, ujenzi wa nyumba za kupangisha, ujenzi wa machinjio ya kisasa kata ya mkundi, na ujenzi wa stendi ya mabasi ya ndani karibu na eneo la SGR Kihonda” alieleza kwa kina, Lubeleje.

Pia, ndugu Lubeleje amesema ili kupunguza adha ya usafiri na mazingira magumu kwa watumishi walioko maeneo ya mbembezoni sana, Manispaa kupitia fedha za mapato yake ya ndani inapanga kununua pikipiki kumi, sita kati ya hizo watakabidhiwa walimu wakuu wa shule za msingi Mbete (1), Sangasanga (2), Ujirani Mwema (2), na Mungi (1), na pikipiki nne watakabidhiwa watendaji wa kata za Bigwa (1), Mkundi (1), Mlimani (1), na Kauzeni (1).

Kwa upande wao wajumbe wa kikao hicho, wamemshukuru mkurugenzi wa Manispaa kwa kuwajali watumishi wa pembezoni na kupanga kuwanunulia pikipiki. Wamemwomba aendelee kuboresha mazingira ya watumishi wake hasa wa pembezoni kwa kukarabati nyumba zao ama kuwajengea mpya.

Aidha, wajumbe hao wamemshauri mkurugenzi wa Manispaa kuhakikisha wanafunzi wa shule za sekondari wanatumia viti na meza badala ya madwati kama inavyoshauriwa na wathibiti ubora wa elimu.

Wameshauri madwati yaliyopo kwenye baadhi ya shule za sekondari yapelekwe kwenye shule za msingi halafu fedha ambayo ingeelekezwa kwenye kuchonga madawati kwa shule za msingi itumike kuchonga meza na viti kwa shule za sekondari ambazo madawati yake yatachukuliwa. 

MWISHO  

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa