• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MEYA KIHANGA AWACHARUKIA WAALIMU WAKUU, AWATAKA WAJITATHIMINI

Posted on: January 19th, 2021

Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amewataka Walimu wakuu wa Shule za Msingi na Sekondari, kujitathimini na kuona Kama wanafaa kukaa Manispaa Morogoro.

Kauli hiyo ameitoa Januari 19, 2021 wakati wa ziara ya kikazi ya ukaguzi wa ujenzi wa vyumba vya Madarasa vilivyojengwa na Manispaa Morogoro na nguvu za wananchi  kufuatia agizo la Serikali la kutaka wanafunzi wote kuingia darasani ifikapo Februari 28.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo, Kihanga, amesema kumekuwa na matokeo mabovu ambayo hayaridhishi jambo linalopelekea Manispaa kushika nafasi za nyuma huku ikiwa mjini.

Mhe. Kihanga, amesema kuwa, sasa ni wakati wa Waalimu hao kuanza kujitathimini upya kutokana na matokeo hayo.

" Nimeanza ziara ya kikazi ya kukagua ujenzi wa Shule na vyumba vya Madarasa, lakini matokeo bado hayaridhishi hususani katika upande wa Sekondari, tunashindwa hadi na wenzetu wa vijijini, sisi tuna kila kitu ila ni wapi tuna kwama? Hizi nafasi sio zetu, niwaombe Waalimu mjitathimini, Serikali inawekeza katika ujenzi na sisi tunataka matokeo mazuri, baada ya ujenzi wa madarasa tunahamia kwenu, kama umeshindwa kukaa Manispaa ondoka kabisa, tunataka matokeo mazuri tufanane na hadhi yetu ya Manispaa" Alisema Mhe.Kihanga.

Aidha aliwataka Waalimu wakuu wanapokaa katika vikao vyao wamualike ili wazungumze kwa pamoja na kuona changamoto ambazo zipo na kuzitatua. Suala la Waalimu amesema kuwa mpango uliopo kwa sasa ni kuongeza Waalimu wa Sayansi ambao ndio changamoto kwa Sasa. Kuhusu Ujenzi wa Shule ya Msingi Konga, amempongeza Sana Mkurugenzi Manispaa Morogoro Sheilla Lukuba, kwa jitihada za kupambania Sekta ya elimu, kwani Sasa amekuwa akitoa fedha nyingi katika kata kwa ajili ya maendeleo mbalimbali ikiwemo sekta ya  elimu.

" Mkurugenzi wetu anajitahidi Sana , tumtumie vizuri, anahangaika Sana, sisi hatuhitaji kubweteka, tufanye kazi, haya matokeo yanatuumiza Sana, Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wote tunaumia, huu ni muda wa kujipanga sasa tutoke hapa tulipo twende mbele"Aliongeza Mhe. Kihanga.

Mwisho , amesema kuwa ziara hizo zitakuwa endelevu, lakini kwanza ameanza katika Shule za Sekondari baada ya hapo atahamia Shule za Msingi. Miongoni mwa Shule alizoanza nazo ziara ni pamoja na Shule ya Msingi Konga Kata ya Mzinga, Shule ya Sekondari Kihonda Kata ya Mazimbu, Shule ya Sekondari Sumaye Kata ya Bigwa na Shule ya Sekondari Lupanga Kata ya Kilakala.

Naye Diwani wa Kata ya Kilakala, Mhe. Marco Kanga, amemshukuru, Mstahiki Meya kwa ziara hiyo huku akimuahidi kumpa ushirikiano na kuhakikisha anafuatilia kwa ukaribu maswala ya elimu katika Kata hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa