• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MILIONI 133. 5 ZA NUFAISHA MIKOPO KWA VIKUNDI VYA WAJASIRIAMALI MANISPAA MORO

Posted on: March 11th, 2019

Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro imetoa mikopo ya kiasi cha Sh milioni 133.5 kwa vikundi 45 vya wanawake ,vijana na watu wenye ulemavu katika mwaka wa fedha 2018/2019 kwa lengo la kuongeza mitaji yao ili kuwawezesha kuzalisha kwa wingi bidhaa mbalimbali na kuongeza vipato vyao kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi katika familia zao.

Ofisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Morogoro, Enedy Mwanakatwe alisema hayo katika risala ya wanawake wa Manispaa ya Morogoro kwa mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Morogoro , Regina Chonjo katika kilele cha maadhimisho ya wanawake Duniani yaliyofanyika ki wilaya  Machi 8 kwenye uwanja wa Jamhuri wa mjini hapa.

Mwanakatwe alisema , kipindi cha mwaka wa fedha 2018/2019 , halmashauri iliweza kutoa mkopo wenye thamani ya Sh milioni 66 kwa vikundi 22 vya wanawake na kiasi kingine cha Sh milioni 37 kwa vikundi 12 vya vijana.

Alisema ,halmashauri imezingatia agizo la Serikali la kutenga asilimia mbili ya mapato yake ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo kwa vikundi vya watu wenye ulemavu na jumla ya Sh milioni 30.5 zimetolewa kwa vikundi 11.

Pia alisema ,kupitia Mfuko wa Jimbo umewezesha Jukwaa la Wanawake kiuchunmi (JUWAKIMAMO), vyerehani 17 na mashine za over lock mbili zenye thamani ya Sh milioni tano ambazo zilikabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini, Abdulaziz Abood , mwishoni mwa mwaka jana .

“ Matarajio ya mradi huu ni kufungua chuo kwa ajili ya mafunzo ya ushonaji kwa wanawake wa Manispaa ya Morogoro wakiwemo vijana wa kike na wakiume wenye uhitaji” alisema Mwanakatwe.

Pamoja na hayo halmashauri ya Manispaa kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii imefanikiwa kusajili vikundi 167 tangu Januari mwaka 2018 hadi kufikia Februari 2019 .

Naye Katibu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) , Wilaya ya Morogoro mjini Kichama, Sofia Kibaba ,aliishauri halmashauri hiyo kuendelea kutenga asilimia 10 ya mapato yake kwa ajili ya makundi hayo na hasa la watu wenye ulemavu ambao wamesahauliwa zaidi na kupatiwa elimu ya masaada wa kisheria kwa wanawake na makundi hayo.

Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Chonjo aliwataka walionufaika na mikopo waitumie kulingana na mahitaji yaliyokusudiwa kwa kuendeleza vikundi vyao kiuchumi.

Pamoja na hayo aliwataka wazazi na walezi wawahamasishe wanafunzi wa kike kupenda masomo ya sayansi ili taifa liweze kuwapata wataalamu wengi wanawake kwenye nyanja za madaktari na wahandisi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa