• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MSIWAFICHE WATOTO WENYE MARADHI YA VICHWA VIKUBWA NA MGONGO WAZI

Posted on: September 10th, 2018

Wazazi  na walezi  wa watoto wenye maradhi ya Vichwa vikubwa na mgongo wazi mkoani Morogoro wameshauriwa kutowaficha ndani watoto hao na badala yake kuwapeleka mapema Hospitali na Vituo vya Afya ili kupatiwa matibabu stahiki kwa ajili ya kuwaondolea matatizo.

Mkuu wa wilaya ya Morogoro, Regina Chonjo alitoa ushauri huo ,hivi karibuni katika hotuba iliyosomwa na Katibu tawala msaidizi wa wilaya ya Morogoro , Yahya Nania ,wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kutoa elimu namna ya kuwahudumia watoto wenye maradhi hayo.

Mafunzo hayo yaliendeshwa na Chama cha wenye watu walemavu wa vichwa vikubwa na mgongo wazi Tanzania (ASBATH) mkoa wa Morogoro na kufanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Morogoro.

Alisema , tatizo hilo linaweza kuepukika endapo akina mama wajawazito watafika kwa wakati katika kliniki kama inavyosahuriwa na madaktari na kupatiwa dawa ya kinga ya tatizo hilo.

“Tatizo hili linaweza kuzuilika kwa mama mjamzito kama atafika kliniki mapema na kupatiwa dawa ya foric Acid kwa kuwa tatizo hili , huanza kwa mama mjamzito kuanzia siku ya 14 hadi 21, hivyo ni muhimu kufika kliniki mapema.” alisema Nania.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro , Dk Frank Jacob alisema kuwa, wanawake wajawazito wakifika mapema hospitalini na vituo vya Afya kutasaidia kupata matibabu na ushauri wa kina na hivyo kupunguza au kutokomeza kabisa tatizo la watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi.

“Watoto hawa wanaweza kutibiwa matatizo haya na kuendelea na shughuli zao kama kawaida endapo watafikishwa mapema Hospitalini kupatiwa tiba , hivyo hakuna haja ya kuwaficha majumbani watoto hawa au kuona tatizo hilo ni laana.” alisema Dk Jacob .

Naye Mwenyekiti Asbath Tawi la mkoa wa Morogoro Colimba Mbiki alisema , tawi lilianzishwa mwaka 2012 na watoto wanne na hadi kimeweza kusaidia watoto 167 kupata tiba kati yao 70 ni wavulana na 63 wasichana , licha ya juhudi hizo lakini watoto 44 wamefariki kwa magonjwa mbalimbali wakiwa na umri wa miaka mitano hadi 10.

Mbiki alisema , chama wanakabiliwa na changamoto kubwa ya usafiri ili kuwafikia walengwa , umbali mrefu wa kwenda hospitali na vituo vya Afya .

Hivyo aliiomba Serikali kuwasaidia kupatiwa huduma ya matibabu katika hospitali za rufaa katika mikoa na vifaa tiba zikiwemo pampasi , mipira ya mkojo , viti vya magurudumu kwa njia ya msamaha.

“ Wazazi wengi wanakosa uelewa na kukata tamaa kuona hali za watoto wao wakidhani wamelogwa au ni mikosi anapopata mtoto mwenye ulemavu huu , kwa hiyo ni kazi kwa viongozi kwenda kutoa elimu ili hatimaye kuwapekela hospitalini “ alisema Mbiki.

Kwa upande wake Mratibu wa Asbath Taifa , Hidaya Alawi ,pamoja na mambo mengine alikabidhi viti vya magurudumu vitano vikiwemo vyenye sehemu ya kujisaidia haja kubwa na ndogo .

Vifaa vingine ni vyandarua jozi 50 , sabuni na sukari ambavyo vimetolewa na Serikali kupita Hospitali ya Muhimbili kitengo cha MOI chini ya Ustawi wa jamii katika hospitali hiyo kwa kushirikiana na chama hicho kwa lengo la kusaidia jamii hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa