• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

NAIBU MEYA MANISPAA YA MOROGORO AFUNGUA MAFUNZO YA MFUMO WA ANWANI ZA MAKAZI KWA MIKOA 13 NA HALAMSHAURI 23 HAPA NCHINI.

Posted on: December 18th, 2021

NAIBU Meya wa Manispaa ya Morogoro, Mhe. Mohamed Lukwele, amefungua Semina ya mafunzo ya Mfumo wa Anwani ya Makazi kwa mikoa 13 na Halamshauri 23 hapa nchini.

Mafunzo hayo yamefunguliwa leo Desemba 18/2021 katika Ukumbi wa CCT uliopo Kata ya Kilakala Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza juu ya mafunzo hayo, Mhe. Lukwele, amesema kuwa utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi na Postikodi unalenga kuharakisha na kurahisisha upatikanaji, utoaji na upelekaji wa huduma ama bidhaa hadi mahali stahiki.

Mhe. Lukwele, amesema kuwa Mfumo wa Anwani za Makazi, unawezesha kufanyika kwa biashara mtandao.

“ Lengo la Serikali ni kuhakikisha kuwa kila Mwananchi, Ofisi ama eneo la biashara linakuwa na Anwani ya Makazi, kwahiyo ili kurahishsa Mfumo huo ni vyema kila Halmashauri ikaweka msukumo katika kujenga uwezo kwa watendaji na wataalamu wa Kata na Mitaa/ Vijiji ikiwa ni pamoja na uwezo katika matumizi ya Programu Tumizi ya Mfumo” Amesema Mhe. Lukwele.

Aidha, amewataka Watendaji wa Vijiji/Mitaa watumike katika kukusanya taarifa za Anwani za Makazi na kutoa Anwani husika kwa Wananchi kwa kutumia Programu Tumizi.

Pia, amewataka Wadau wakiwemo Wananchi wahamasishwe kujiwekea miundombinu wa mfumo katika maeneo yao ya Makazi, Ofisi ama eneo la biashara.

Aidha, ameipongeza Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari kwa kujenga uwelewa kwa Viongozi kuanzia Wakuu wa Mikoa, Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi wa Halamshauri zote nchini pamoja na Mameya/ Wenyeviti wa Halamshauri huku akisema hatua hiyo ya kushirikisha kada zote itaharakisha utekelezaji wa Mfumo wa Anwani za Makazi.


Mwisho, amesema kutokana na umuhimu wa Anwani za Makazi katika Nyanja zote za Kiuchumi na Kijamii, ni vyema suala la Anwani za Makazi iwe ajenda ya kudumu katika vikao vya ngazi zote ili kuchochea utekelezaji na matumizi ya mfumo.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhandisi Clarence Nchwekeleza, amesema kuwa amesema Mfumo wa Anwani za Makazi utaisaidia Serikali kupanga mipango ya Maendeleo, kuimarisha usalama, kuongeza ajira na Mapato ya Serikali.

Eng. Nchwekeleza, amesema mfumo huo utaendana na programu tumizi (mobile application) ya mfumo wa anwani za makazi ambayo itakayorahisisha matumizi na utekelezaji wa mfumo kwa kuzingatia kwamba itatumika katika kukusanya taarifa za Barabara, wakazi, makazi pamoja na kutoa anwani za makazi ya wananchi,kaya, ofisi na eneo la biashara.

“Dhamira ya Wizara kila mwananchi anakuwa na anwani yake ya makazi katika eneo analoishi, eneo la ajira au eneo la biashara, nitoe wito kwa watendaji, viongozi na wataalamu hususani wa kata na mitaa wajengewe uwezo wa kutosha ili waweze kuwa na uelewa wa pamoja,waweze kuratibu, kusimamia na kutekeleza mfumo huu” Amesema Eng. Nchwekeleza,

Aidha,amesema kwa kutumia utaratibu huu wa anwani za makazi, mpango shirikishi ulioandaliwa baina ya Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Ofisi ya Taifa ya Takwimu na Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Zanzibar wa kutekeleza zoezi hili utasaidia sensa ya watu na makazi ya mwakani kufanyika vizuri sana kwa sababu pia itaonyesha wananchi wanapokaa na wanafanya kazi gani.

Miongoni mwa Mikoa 10 inayo jumuisha Halmashauri 23 iliyoshiriki katika Mafunzo hayo ni pamoja na Jiji la Dar Es Salaam, Mwanza , Mbeya, Arusha, Tanga, Dodoma na Mikoa ya Morogoro,Mara, Kagera, Pwani , Iringa, Shinyanga na Geita.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa