• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC SANARE AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO MANISPAA YA MOROGORO.

Posted on: February 28th, 2020

MKUU wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Loata Sanare, amefanya ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro ikiwa na lengo la kuboresha kasi ya uwajibikaji na upatikanaji mzuri wa huduma kwa wananchi.

Ziara hiyo imeanza leo Februari 28 , 2020 katika Kata ya Mlimani ikiwa ni moja ya ziara zake ambazo analenga kuzifanya katika Kata zote 29 zilizopo Manispaa ya Morogoro.

Akizungumza na Waandishi wa habari, RC Sanare, ameanza ziara yake katika Shule ya Msingi  Benard Bendel isiyo ya Serikali iliyopo Kata ya Kichangani kufuatia maagizo aliyoyatoa katika Uongozi wa shule hiyo kuhusiana na ukarabati wa miundombinu  ya Bweni la Wanafunzi wa Kiume .

Aidha, RC Sanare, baada ya ukaguzi huo wa bweni amejidhirisha kwamba maagizo aliyoyatoa yamefanyiwa kazi na sasa Bweni hilo lipo tayari kwa ajili ya matumizi kwa wanafunzi.

"Nipo hapa shuleni kwa ajili ya kuangalia nilichokiagiza, kwakweli hali haikuwa nzuri katika Bweni la wanafunzi hivyo katika kikao changu nilimuagiza Mwalimu Mkuu kuhakikisha yale mapungufu yaliyopo katika Bweni la wanafunzi wa Kiume yanafanyiwa kazi na sasa nimejiridhisha kwa macho yangu kwamba hakuna shida tena , napenda kusema sasa rasmi wanafunzi wanawezakulitumia bweni hilo lakini pale mnapoona kuna shida na mnataka msaada wa Kiserikali msisite  kutuambia nasi tutawapatia ushirikiano  lengo ni kuboresha  elimu katika Shule zetu zilizopo katika Mkoa wetu wa Morogoro na umeniambia una shule nyingine usisite nitakuja kikubwa nenda kaweke mazingira vizuri "Amesema RC Sanare.

Pia amesema lengo la kufanya ziara katika shule binafsi ya Bernard Bendel ni kuhakikisha kwamba wana boresha miundombinu ili kuongeza viwango vya ufaulu kwani katika takwimu za viwango vya ufaulu katika ngazi za Mkoa  hawaangalii shule za Serikali pekee bali waangalia matokeo kwa ujumla katika Mkoa mzima.

Pia amemuagiza Mhandisi wa Manispaa ya Morogoro kusimamia majengo ya Shule kikamilifu kuanzia shule za Serikali pamoja na zile binafsi pamoja na kusisitisha ujenzi kwa kuweka alama ya X majengo yote ambayo yanajengwa bila ya vibali vya ujenzi.

Katika ukaguzi huo wa maendeleo shuleni, hakuishia katika shule hiyo pekee bali amepata nafasi ya kutembelea Shule ya Sekondari Bungodimwe iliyopo Kata ya Mlimani na  kukagua Ujenzi wa vyumba viwili vya Madarasa vilivyomalizika na kugharimu shilingi Milioni 25 na laki 9.

Amesema kuwa, kwa jinsi Ujenzi huo ulivyokamilika ameridhika na ujenzi huo na kusema thamani ya pesa inaonekana huku akiwapongeza sana Wananchi kwa jitihada walizozionesha aidha amesema bado nguvu za Wananchi zinahitajika ili kuendelea kutanua miundombinu ya shule hiyo Ikiwemo ukarabati wa Madarasa, ujenzi wa Jengo la Utawala , Maabara pamoja na Ofisi ya Mkuu  wa Shule.

Pia amewataka TARURA ,  kuichonga barabara hiyo inayowaunganisha wananchi wa Towelo yenye urefu wa KM 3.5 kutoka kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

"Ndugu zangu TARURA mliniambia kwamba mlishaipitisha barabara hii katika Bajeti ya Mwaka 2020/2021 lakini mpaka leo sioni utekelezaji, sijaridhishwa na majibu yenu ya kupunguza bajeti kwahiyo hao viongozi wenu wa Makao Makuu wakija naomba nikutane nao na niwalete waone kama watapunguza   laa, ombi langu ni kwamba iangalieni hii barabara kwa jicho la huruma ili kunusuru watoto wetu kuacha utoro, wanafunzi kufika kwa urahisi na wananchi pia kunufaika na huduma hii muhimu" Amesisitizia RC Sanare.

Kwa upande Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Mhe. Regina Chonjo, ameiomba TARURA kuwapatia njia nzuri ili magari yaweze kufikika katika Shule hiyo ili kurahisisha usafiri kwa Walimu na Wanafunzi pamoja na Wananchi wanaoitumia barabara hiyo japo sio kwa kiwango cha  lami lakini hata kuchonga sehemu korofi itasaidia.

"Barabara hii ni muhimu sana , hivyo mkiitengeneza vizuri itakuwa si mkombozi wa wanafunzi pekee bali hata kwa wananchi wanoitumia barabara hii watanufaika na huduma hii ya barabara , walimu watakuja shuleni, utoro kwa wanafunzi  utapungua kutokana na taarifa iliyotolewa na Mkuu wa Shule hii ya Bungodimwe,  na wakazi wa huku wataitumia kwa ajili ya kusafirisha bidhaa zao na kwenda pamoja na kurudi majumbani "Amesema DC Chonjo.

Aidha RC Sanare amewataka Wanafunzi wasome kwa bidii na kuacha kucheza ili waweze kutimiza ndoto zao katika maisha na kuwa Viongozi bora wa Taifa ili kubadilisha maendeleo hususani watoto wa kike kwani viongozi wengi wa kike duniani ni kwamba wameaminiwa kulingana na elimu zao.

Pia RC Sanare,ameahidi kuchangia shilingi Milioni Moja pamoja na Mkuu wa Wilaya shilingi laki 5 kwa ajili ya uboreshaji wa maendeleo katika shule hiyo.

Amesema Wazazi Katika kata  hiyo ni wagumu kuchangia elimu lakini furaha yake ni kuona baada ya miaka 5 au 10 viongozi wa Morogoro wanapatikana katika Shule za Morogoro.

Katika hatua nyingine, amewataka Watendaji wa Halmshauri ya Manispaa ya Morogoro kuanzia ngazi za Mitaa na Kata wawe na utaratibu wa kusoma mapato na matumizi katika vikao vyao wanapokuatana na wananchi kwani suala hilo lipo kisheria na agenda kubwa ziwe ni kujadili ulinzi na usalama pamoja na mapato na matumizi kabla hawajaingia katika ajenda mpya.

Agizo hilo amelitoa kufuatia malalamiko ya wananchi katika kikao cha wazi kilichofanyika katika Ofisi ya Kata ya Mlimani huku baadhi ya wananchi wakilalamikia Uongozi wa Kata pamoja na Mitaa kutosoma mapato na matumizi jambo linalowapelekea kutokuwa na uelewano mzuri kati ya wananchi na viongozi wa kata hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, amempongeza Raisi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli kwa kuwapatia fedha shule zote za Manispaa ya Morogoro kupitia mpango wa Elimu bure bila malipo pamoja na pesa za miradi ya maendeleo hususani miradi  ya kimkakati ,  Mkuu  wa mkoa Morogoro Mhe. Loata Sanare kwa  hatua za kuboresha maendeleo ya elimu  , Mkuu wa wilaya ya Morogoro Mhe. Regina Chonjo ya usimamizi mzuri wa miradi  na kazi kubwa na nzuri wanazozifanya ili kuwaletea maendeleo wananchi.

Aidha amepongeza  juhudi kubwa zinazofanywa na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mhe. Abdulaziz Abood kufuatia kutoa pesa nyingi za mfuko wa Jimbo pamoja na pesa zake binafsi katika kuchangia maendeleo ya Manispaa  ya Morogoro.

Naye Mstahiki meya wa Manispaa ya Morogoro, mhe. Pascal Kihanga, amesema shule za Manispaa ya Morogoro zinakabiliwa na changamoto nyingi hivyo amemuomba  Mkuu wa Mkoa kueleza na kuwapa maelekezo pale anapoona kuna makosa ili wajirekebishe kuliko kuyaacha na kuwagharimu baadae.

Kihanga, amewataka Wazazi kuendelea kuchangia pesa na vifaa mbalimbali ili kuleta maendeleo katika shule hiyo.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa