• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

RC SHIGELA AIPONGEZA MANISPAA YA MOROGORO KUPATA HATI SAFI MWAKA WA FEDHA 2019/2020

Posted on: June 16th, 2021

MKUU wa Mkoa wa Morogoro , Mhe. Martine Shigela, ameipongeza Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo kutoka mwaka 2015/2016 mpaka mwaka 2019/2020.

Pongezi hizo zimetolewa  Juni 16/2021 katika kikao maalum cha Baraza la madiwani cha kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka 2019/2020, kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Soko Kuu la Chifu Kingalu Morogoro.

Sambamba na pongezi hizo, RC Shigela, amewasifu watendaji wa Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana na Baraza la Madiwani kwa utendaji wao mzuri wa kazi na kujituma kwa kuwahudumia wananchi wa Manispaa ya Morogoro.

"Ninampongeza Mkurugenzi na watendaji wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kwa kushirikiana vyema na Baraza la Madiwani kwa utendaji kazi mzuri ulioleta matokeo mazuri na kuiwezesha Halmashauri kupata hati safi kwa kipindi cha miaka mitano mfululizo.”

Aidha, RC shigela, ametoa rai kwa watumishi wote wa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro kutumia utaalamu wao katika utendaji kazi wao na pia kufanya kazi kama timu moja katika kuwahudumia wananchi.

Vilevile amewataka kusimamia vyanzo vya mapato vilivyopo ndani katika kuongeza mapato ya Halmashauri na sio kutegemea vyanzo vya nje.

Aidha ametoa wito kwa wakuu wa Idara kutoa mafunzo ya kazi kwa vitendo(On job Training) ya mara kwa mara kwa watendaji wao ili kuhakikisha kazi zinafanywa vizuri na kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, RC Shigela, amewataka watendaji wasiopeleka fedha benki wapeleke kwa wakati na wasiofanya hivyo waweze kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Hata hivyo ,ameagiza kufungwa kwa mfumo wa uhakika wa mapato kwenye Stendi ya mabasi ya Msamvu pamoja na kusimamia vyanzo vikubwa vya mapato ambapo hadi kufikia Agosti mwaka 2021 mfumo huo uwe umeshakamilika.

Pia amezitaka Taasisi za Serikali kuacha tabia ya kupelekana Mahakamani jambo ambalo amelipinga vikali huku akizitaka Taasisi hizo ambazo zinakesi wahakikishe ndani ya wiki moja wamefuta kesi hizo na kufanya majadiliano yao nje ya mahakama.

Hata hivyo,amesema yupo katika hatua ya kukutana na wakazi wanaoishi katika eneo la Star City kabla ya kukutana na mmiliki wa eneo hilo ili kuweza kujadiliana nao na kuona jinsi ya kuweza kuondoa changamoto zinazowakabili .

Aidha, amewataka watendaji na watumishi kuhakikisha kwamba wanapatia ushirikiano mzuri Madiwani wapotaka kuongea na wananchi wao katika kutatua kero na changamoto za wananchi.

Mwisho RC Shigela, ameutaka Uongozi wa Manispaa ya Morogoro kuhakikisha kwamba wanayashughulikia magari yote ambayo ni mabovu kwa kuyafanyia matengenezo ili yaweze kufanya kazi pamoja na kupitia mkataba wa Kampuni ya usafi wa Kajenjere ili kuona namna gani ya kuweza kutatua changamoto ambazo wananchi wamekuwa wakizielekeza kwao.

Kwa upande wa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Morogoro na Diwani wa Kata ya Mazimbu , Mhe. Pascal Kihanga, amewataka watendaji kujitahidi kukusanya mapato pamoja na kuweka utaratibu mzuri wa kuweza kushughulikia changamoto za wafanyabiashara wa Soko Kuu la Chifu Kingalu.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa