• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANAWAKE WA JIWA WASAIDIA WAATHIRIKA WA MAFURIKO MOROGORO

Posted on: February 7th, 2024

Wanawake wameendelea kujitokeza kutoa msaada wa mahitaji ya msingi kwa wananchi wa Manispaa ya Morogoro, walioathiriwa na mafuriko yalitokana na mvua nyingi zilizonyesha hasa tarehe 24.01.2024.

Leo, tarehe 06.02.2024, wanawake wa kikundi cha Jiendeleze Women Association (JIWA), chenye Ofisi yake kwenye kata ya Kihonda, wamemkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, mheshimiwa Rebbeca Nsemwa kilo 175 za unga wa ugali, sabuni za miche na za unga, pamoja na nguo na viatu ikiwa ni msaada wao kwa waathirika wa mafuriko.

Mheshimiwa Nsemwa amewashukuru sana wanawake hao wajasiriamali kwa tendo lao la huruma kwa wananchi wake na ametoa wito kwa ye yote atakayeguswa kuendelea kujitokeza kutoa misaada kwa ajili ya wananchi wenzetu ambao baadhi yao nyumba zao zilibomoka, na wengine vitu vyao  vyote vilisombwa na maji vikiwemo vyakula na mavazi.

“Ninyi ni kundi la pili la wanawake mliokuja kutoa msaada kwa ndugu zetu. Kundi la kwanza lilikuwa la Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT). Salamu zenu hizi nitazifisha kwa Mkuu wetu wa Mkoa pia. Binafsi nimefurahi sana kupokea kundi hili, na ninatoa wito kwa wanaume nao wajitokeze” alisema mheshimiwa Nsemwa.

Mwenyekiti wa kikundi hicho, Bi. Doroth Luoga amesema dhumuni la kikundi chao ni kusaidiana wao kwa wao na kusaidia jamii inayowazunguka. Baada ya kuona jinsi wananchi wenzao walivyoathiriwa na mafuriko, walikubaliana kuchangishana ili kutoa mkono huo wa pole.

Naye mratibu waMaafa wa Manispaa ya Morogoro, ndugu Elizabeth Badi amesema kwa sasa kipaumbele cha misaada hiyo ni kwa wananchi wenye hali duni kiuchumi, ambao wameathiriwa na mafuriko.

“Unajua miongoni mwa walioathiriwa na mafuriko, wapo watu ambao mafuriko ni kana kwamba yamekuja kuwaongezea ugumu wa maisha na hawana pa kushika. Hao ndio ambao kwa sasa misaada hii tunaielekeza kwao” alifafanua Badi.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa