• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

WANUFAIKA WA TASAF MANISPAA WATAKIWA KUTOBWETEKA NA MAFANIKIO WALIYOYAPATA

Posted on: January 16th, 2020

MRATIBU  wa TASAF Halmshauri ya Manispaa ya Morogoro, Feliciana Katemana,  amewataka Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaotekelezwa na Serikali kupitia TASAF kutumia fursa hiyo kwa ukamilifu kwa kufanya kazi kwa bidii  ili  kutimiza azma ya serikali ya kupambana na umaskini nchini.

Hayo ameyasema leo Januari 16. 2020 wakati akikagua na kujionea utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo wa Maendeleo ya Jamii-TASAF katika Kata ya Mwembesongo.

Amesema  Serikali ya Awamu ya Tano inafanya juhudi kubwa za kuweka mazingira mazuri kwa  Wananchi kujiletea maendeleo na kuboresha maisha yao hivyo akawataka kutumia vizuri fursa hiyo kwa kufanya kazi za uzalishaji mali kwa bidii ili kukuza uchumi wao na hatimaye kuchangia katika pato la taifa na kuondoa kero ya umaskini miongoni mwao kwa vitendo.

Amesema kuwa Manispaa ya Morogoro katika mradi wa TASAF imepokea jumla ya Shilingi Milioni 119 ambazo zilikuwa ni za kipindi cha Mwezi Machi na Aprili kwa mwaka jana 2019 huku akiwataka Wananchi kuwa na subira kwani Serikali yao ni tulivu na itawapatia watu wote walio na sifa katika mradi huo bila ubaguzi wa aina yoyote.

Hata hivyo amesema kuwa , fedha hizo zimegawiwa kwa walengwa wapatao 2945 katika kata zote 29 za Manispaa ya Morogoro katika Mitaa 164.

Katemana amewataka Walengwa wa TASAF kutobweteka na mafanikio waliyoanza kuyapata kutokana na huduma zinazotolewa na Serikali kupitia TASAF badala yake waendelee kuuchukia umaskini kwa vitendo kwa kufanya kazi kwa bidii ili  hatimaye waweze kuboresha maisha yao huku akisisitiza ustawi wa jamii kwa ujumla hususani watoto kama ilivyo dhamira ya Serikali.

Katika hatua nyingine , Katemana , amewashauri maafisa maendeleo na ustawi wa jamii wanaosimamia mpango wa TASAF katika ngazi za Kata kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu mkubwa na kuzingatia  Uzalendo kwani amesema Mfuko huo unagusa nyanja muhimu za Maendeleo ya Wananchi katika sekta mbalimbali zikiwemo elimu, afya,maji,uchumi,kilimo,mifugo na hifadhi ya mazingira na hivyo kuwa miongoni mwa sekta zinazogusa maisha ya wananchi wengi moja kwa moja.

“Serikali inathamini mchango wa taasisi hii katika jitihada zake za kupunguza umaskini nchini, endeleeni kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yaliyokusudiwa kwa haraka na ufanisi mkubwa” amesisitiza Katemana.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Sheilla Lukuba, amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika utekelezaji wa shughuli za Mfuko huo yaliyochangiwa kwa kiwango kikubwa na Serikali,Wadau wa Maendeleo na Wananchi hususani Walengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ambao amesema kwa sehemu kubwa wameanza kuboresha maisha yao na kuonyesha namna wanavyouchukia umaskini kwa vitendo.

Kwa upande wake, mnufaika wa mpango wa kunusuru kaya maskini ,  Bunga Mogela, ameishukuru Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mhe. Rais Magufuli huku akikiri kuwa  mpango huo umekuwa mkombozi mkubwa kwao kwani umeweza kuwabadilisha kimaisha na kuiomba serikali kuongeza kiwango cha ruzuku ili kilingane na thamani halisi ya fedha kwa sasa.

Naye Antari Shadadi,  mkazi wa kata ya Mwembesongo, amesema kuwa kwa sasa anajishughulisha na ununuzi wa Mkaa pamoja na kusomesha Watoto kupitia biashara hiyo huku akimuomba Mhe. Rais Dkt. John Magufuli kuendelea na moyo huo huo wa kuwasaidia walala hoi na watu wenye vipato vya chini katika Kaya Masikini.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa