• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MAPOKEZI YA MBIO ZA MWENGE WA UHURU 21/07/2018

Wednesday 4th, June 2025
@HALMASHAURI YA MANISPAA YA MOROGORO

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MAPOKEZI YA MWENGE WA UHURU KATIKA WILAYA YA MOROGORO

  • Ndugu wananchi,

Mimi Regina Reginald Chonjo, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro napenda kuwaarifu kuwa kama ilivyo ada Mwenge wa Uhuru hukimbizwa kila mwaka katika Wilaya zote za Jamhuri ya muungano wa Tanzania Bara na Visiwani, katika kipindi chote umekuwa ni kichocheo cha maendeleo. Napenda kuwataarifu kuwa Mwenge wa Uhuru ambao hukimbizwa Nchi nzima tutaupokea Wilayani Morogoro tarehe 21.7.2018 ukitokea Mkoani Pwani. Tutaupokea Bwawani, mpakani mwa Mikoa ya Pwani na Morogoro.

Kwa Wilaya yetu, Mwenge wa Uhuru unategemea kuona, kuzindua na kuwekwa mawe ya Msingi katika miradi ya maendeleo katika Nyanja mbalimbali.

Ndugu wananchi wa Wilaya ya Morogoro, ninayo furaha kubwa kwa mapokezi mazuri ya Mwenge wa Uhuru mwaka jana na kuiwezesha Wilaya yetu ya Morogoro Mjini kushika nafasi ya kwanza Kimkoa mwaka 2017. Hii ilitokana na ushirikiano wa pamoja na mshikamano mliouonesha. Nawashukuru sana, naomba tushirikiane tena mwaka huu kuilinda na kuitetea nafasi yetu. Ushindi unatokana na muitikio wenu kwa wingi, uchangamfu, ukarimu na muonekano wa miradi yetu ya maendeleo ambayo sina wasiwasi na ubora wake (value for money).

Ndugu wananchi, kwa Manispaa ya Morogoro napenda kuwajulisha kuwa mkesha wa mbio za Mwenge utafanyika katika viwanja vya Kiwanja cha Ndege ambapo maonesho ya vikundi mbalimbali yatafanyika sambamba na burudani za vikundi mbalimbali vya sanaa na muziki vitakuwepo na hatimaye tunategemea kuukabidhi Wilaya ya Gairo siku ya Jumapili Asubuhi tarehe 22/07/2018.

Pia tarehe 24.7.2018, Mwenge wa Uhuru utapokelewa Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ukitokea Wilaya ya Mvomero na kukimbizwa katika miradi ya Tarafa ya Mikese na kukabidhiwa Halmashauri ya Ifakara tarehe 25.7.2018.

  • Mwenge wa Uhuru ni Tunu ya Taifa,
  • Mwenge wa Uhuru ni hazina kubwa tuliyoachiwa urithi na Baba yetu wa Taifa Mhe. Mwl. Julius Kambarage Nyerere.
  • Mwenge wa Uhuru unakimbizwa Tanzania kutukumbusha Uhuru na Amani tuliyonayo Watanzania.

Unawashwa ili ulete Matumaini, maendeleo, maisha mazuri, usalama, heshima, utu wa Binadamu bila ubaguzi wa Dini, kabila, wenye nacho na wasionacho.

Kauli mbiu 2018:- ELIMU NI UFUNGUO WA MAISHA: WEKEZA KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU. 

Kauli Mbiu hii inaenda sambamba na Juhudi za Mhe. Rais John Pombe Magufuli:-

  • Elimu Bila malipo na miradi mingi ya maendeleo ambayo ni:-
  • Uchumi wa Viwanda.
  • Treni ya Mwendokasi.
  • Barabara/ madaraja / Boti, maji (Bwawa la Kidunda).
  • Nishati – REA, Bonde Mto Rufiji maarufu Stiglers Gauge.
  • Ndege za kisasa Bombadee kufufua Shirika la Ndege ATCL.
  • Kupanua Bandari Dar es Salaam.
  • Bomba la mafuta Tanga – Uganda.
  • Afya Hospitali za Wilaya.

Ili maendeleo haya na Juhudi hizi za Mhe. Rais ziweze kufanikiwa na kuzaa matunda zitahitaji wananchi wenye Elimu:- wahandisi, Daktari, Prof, wachumi, wahasibu, wataalam Rasilimali watu, marubani nk.

Ndugu wananchi wa Wilaya ya Morogoro, shimeshime kwa heshima kubwa na taadhima naomba kama kawaida yetu tujitokeze kwa wingi kuulaki Mwenge wetu wa Uhuru.

ASANTENI KWA KUNISIKILIZA, NAWATAKIA MAANDALIZI MEMA YA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU.

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI YATOLEWA MANISPAA YA MOROGORO.

    May 14, 2025
  • BALOZI BATILDA ATAKA MAONI YA WADAU KUFANYIWA KAZI KUELEKEA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MSHARIKI 2025

    May 06, 2025
  • MAAFISA ARDHI WATAKAOBAINIKA NI VYANZO VYA MIGOGORO YA ARDHI TUTAWAFIKISHA MAHAKAMANI-DKT.NDUMBARO.

    May 05, 2025
  • WAAJIRI SEKTA BINAFSI RUHUSUNI WATUMISHI WENU KUJIUNGA NA CHAMA CHA WAFANYAKAZI - RC MALIMA.

    May 01, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa