• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MIZENGO PINDA AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MASHARIKI,ASISITIZA USHIRIKIANO.

Posted on: August 8th, 2025

Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya nne ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mizengo Kayanza Peter Pinda, amefungua rasmi maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki huku akitoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na kupeana uzoefu na mawazo yatakayoleta mabadiliko katika sekta za kilimo, mifugo na uvuvi.

Mhe. Pinda amesema hayo Agosti 2, 2025, wakati akifungua maonesho ya wakulima, wafugaji na wavuvi (Nanenane) yanayofanyika katika viwanja vya Mwl. Julius Kambarage Nyerere mkoani Morogoro, ambapo kaulimbiu ya maonesho hayo inasema, “Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, 2025”.

Mhe. Mizengo Pinda amesema kuna umuhimu wa sekta binafsi na umma kuwa na ushirikiano wa karibu na kufanya kazi pamoja hususan katika nyanja za ufugaji, kilimo na uvuvi ili kuweza kuongeza thamani ya mnyororo wa mazao yatokanayo na sekta hizo kwa maslahi mapana ya taifa.

“Niwaombe sana wananchi: ushirikiano, ushirikiano miongoni mwetu; jambo la msingi sana,” amesema Mhe. Mizengo Pinda.

Aidha, Mhe. Pinda amesema ili kuwaletea maendeleo watanzania, lazima kuishirikisha Sekta binafsi kwa kuwapatia maeneo ya uwekezaji, Pia amewataka wananchi kuachana na jembe la mkono badala yake watumie zana bora za kilimo, mifugo na uvuvi zinazooendana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia.

Sambamba na hayo, Mhe. Mizengo Pinda amebainisha mazao yaliyoongoza kuingiza fedha kupitia mauzo ya nje hivyo kuchangia pato la Serikali kwa kipindi cha mwaka 2022 hadi 2025 kuwa ni pamoja na zao la ufuta limeingiza zaidi ya sh. trilioni 2.2, korosho sh.Bil. 931, tumbaku zaidi ya sh. Bil. 800, na mengine yaliyoongezwa thamani kupitia mfumo wa stakabali za ghala.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu huyo Mstaafu amewakumbusha wananchi kujitokeza na kushiriki uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, kwani ni haki yao ya Msingi kumchagua viongozi wao ili waweze kuwaletea maendeleo katika maeneo yao.


Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima, amemshukuru Mhe. Pinda kwa kukubali kushiriki ufunguzi wa maadhimisho hayo, pia amesema wataendelea kujipanga kuhakikisha maonesho yajayo yanakuwa mazuri kuliko yaliyopita.

Maonesho ya Nanenane Kanda ya Mashariki kwa mwaka huu wameandaa jukwaa la mafunzo ya mbinu bora za kilimo, mifugo na uvuvi, hivyo wananchi na wadau mbalimbali wameaswa kufika na kupata elimu ya sekta hizo ili ziweze kuleta tija zaidi.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 04, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 14, 2023
  • ENVIRONMENT AND SOCIAL IMPACT ASSESSMENT April 24, 2024
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • MIZENGO PINDA AFUNGUA MAONESHO YA NANENANE KANDA YA MASHARIKI,ASISITIZA USHIRIKIANO.

    August 08, 2025
  • MHAKIKI WA MASHINDANO YA AFYA NA USAFI WA MAZINGIRA MWAKA 2025 AMPONGEZA MKURUGENZI MANISPAA YA MOROGORO KWA UWEKEZAJI KATIKA SEKTA YA AFYA NA USAFI.

    August 07, 2025
  • MANISPAA YA MOROGORO YAADHIMISHA WIKI YA UNYONYESHAJI WA ZIWA LA MAMA

    August 07, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI WASAIDIZI WA UCHAGUZI NGAZI YA KATA JIMBO LA MOROGORO MJINI YAFUNGWA RASMI

    August 06, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa