• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC NSEMWA AKABIDHI OFISI KWA DC KILAKALA ,AACHA UJUMBE KWA VIONGOZI

Posted on: August 22nd, 2024

Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Morogoro ambaye kwa sasa ni Mkuu wa Wilaya ya Bahi,Mhe.Rebeca Nsemwa, amekabidhi rasmi Ofisi kwa Mkuu mpya wa Wilaya ya Morogoro Mhe.Mussa Kilakala.

Makabidhiano hayo ya Ofisi yamefanyika Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na badae amefanya mkutano na kuzungumza na watumishi wa Manispaa ya Morogoro Agosti 21-2024 kwenye Ukumbi wa Manispaa ya Morogoro.

DC Nsemwa, amewashukuru Viongozi wa Chama wa Wilaya na Mkoa, Viongozi wa Halmashauri za Manispaa ya Morogoro na Halmashauriya Wilaya ya Morogoro ,Madiwani wa Halmashauri zote , Kamati ya ulinzi na Usalama, Watumishi wa Wilaya hiyo na Viongozi wa Dini na Mila na Wananchi kwa Ushirikiano waliompa kipindi cha uongozi wake na kuwataka kushirikiana na Mkuu mpya wa Wilaya hiyo ya Morogoro.

Aidha,DC Nsemwa,amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan, kwa kuendelea kumuamini katika utendaji

Pia,amemuomba Mkuu wa Wilaya Mhe.Kilakala, kuhakikisha anafanikisha ndoto ya Manispaa kuwa Jiji pamoja na kukabiliana na changamoto ambazo ni maji,miundombinu pamoja na suala la usafi japo tayari hatua zimechukuliwa za kuweka Mji safi.

"Kaka yangu Kilakala ni mzoefu sana ,mwadilifu na mchapakazi naombeni mumpe ushirikiano kama mlivyonipa mimi, hakikisheni pia Viongozi mnaendelea kukemea vitendo vya ukatili wa kijinsia "Amesema DC Nsemwa.

Naye Mhe.Kilakala,ambaye ndiye Mkuu mpya wa Wilaya ya Morogoro, ametoa dira ya Wilaya kuwa itajikita katika ushirikiano wa kutatua changamoto zinazowakabili wananchi ili kuharakisha Maendeleo Wilayani humo ikiwemo usalama wa raia na mali zao, mahusiano kati ya Madiwani,watumishi na Mkurugenzi ambapo mahusiano hayo yatasaidia sana kufikia malengo na hatimaye ndoto ya Manispaa ya Kuwa Jiji inakamilika.

DC Kilakala, amewataka Watumishi kuchapa kazi kwa bidii na kutoa wito kwa wananchi kuendelea kushirikiana na Serekali katika suala la maendeleo.

Aidha, DC Kilakala, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kumuamini na kuahidi kumwakilisha vyema kwa kutatua changamoto za Wananchi na kusimamia shughuli za Maendeleo.

Kuhusu eneo la Afya,DC Kilakala,amesema Mji wa Manispaa unapokea wageni wengi hivyo umakini unahitajika katika kutoa huduma ili kuepuka magonjwa ya milipuko pamoja na wajawazito na Wazee kupewa vipaumbele katika vituo vya kutolea huduma za afya .

Kuhusu Wamachinga, amesema watashauriana namna bora ya kuhakikisha machinga wanakuwa salama na shughuli zao.

Amesema kwa sasa kuna fursa ya mradi wa SGR, hivyo kuna haja ya kuwa na Kituo cha Stop Center chenye huduma mbalimbali zitakazosaidia kuongeza mapato katika Halmashauri.

Mwisho,Mhe.Kilakala,amesema ipo haja ya kuanzisha "MOROGORO SAMIA FESTIVAL"katika kupongeza juhudi za Rais Dkt.Samia za kuipatia Morogoro fedha nyingi za miradi ya Maendeleo.

Akizungumza kwa niaba ya Watumishi wa Manispaa, na Madiwani kwa ujumla, Meya Manispaa ya Morogoro, Mhe. Pascal Kihanga, amewapongeza Wakuu hao wa Wilaya kwa kuendelea kuaminika na kuteuliwa katika nyazifa hizo pia ametumia fursa hiyo kumkaribisha Mhe. Kilakala kuwa wamepokea maelekezo watashirikiana kikamilifu kuiletea Manispaa ya Morogoro Maendeleo.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa