• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

DC NSEMWA AZUNGUMZA NA VIJANA WA MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: April 23rd, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Morogoro mheshimiwa Rebbeca Nsemwa, amewataka vijana kuwa wazalendo kwa kufanya mambo yenye faida kwa nchi, na yanayotetea maslahi ya nchi huku wakiepuka kutumia maendeleo ya kiteknolojia kupotosha maadili ya kitanzania.

Nsemwa ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na vijana wanaotarajiwa kushiriki kwenye mdahalo utakao fanyika kwenye usiku wa mkesha wa Mwenge wa Uhuru Jumamosi, tarehe 27.04.2024 katika uwanja wa shule ya msingi K-Ndege Manispaa ya Morogoro.

Amewataka vijana kuchangamkia fursa ya mikopo ya asilimia kumi inayotolewa na Halmashauri, kwa kuwa mikopo hiyo itawasaidia kujikwamua kiuchumi na kupambana na changamoto ya ajira, inayowakabili vijana wengi hivi sasa.

Katika hatua nyingine mheshimiwa Nsemwa ameitaka jamii kuwa karibu na vijana, na kuwapa malezi bora ili kuwalinda na mambo yanayoweza kuleta madhara makubwa kwa Taifa na nguvu kazi yake kwa ujumla, ikiwemo suala la mahusiano ama ndoa za jinisia moja.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Morogoro ndugu Emmanuel Mkongo, amewataka vijana kuwa na mtazamo chanya kuhusu Mwenge wa Uhuru, na kuhakikisha wanachangamkia fursa zinazopatikana ndani ya mkoa wa Morogoro hasa katika sekta za kilimo na uvuvi.

 “Msiutazame Mwenge wa Uhuru kama utambi unaowaka na kutoa moshi, bali tambueni kwamba wenyewe ni tunu ya Taifa letu, inayohamasisha masuala ya uzalendo, upendo, amani na utulivu.

“Kila mara Mwenge wa Uhuru unapopita kwenye maeneo yote nchini huwa unasisitiza dhima ya Taifa, ya kupambana na rushwa na dawa za kulevya, ambazo hivi karibuni zimekuwa zikichangia sana kuathiri afya ya akili ya vijana wanaozitumia” alieleza Mkongo.

Aidha, Mkongo amewataka vijana kutumia mdahalo huo kupata mawazo chanya na maarifa mapya, yatakayo wajenga, kupata stadi za maisha na kujadili nchi yetu ilikotoka na inakokwenda, kwa sababu wao vijana wanalo jukumu kubwa la kuhakikisha nchi inasonga mbele.

Naye msimamizi mkuu wa mdahalo huo, Dkt. Massimba amewaasa vijana kuacha kualalamika mitaani, badala yake wazingatie uzalendo na wajue stadi za maisha za sasa ili waweze kutimiza ndoto zao.

Dkt. Massimba ametaja uadilifu, uaminifu, ukengeufu dhidi ya tamaduni na imani zetu, uongozi, uzalendo,rushwa, dawa za kulevya, na stadi za maisha kuwa ndizo mada zitakazo jadiliwa kwenye mdahalo huo wa usiku wa tarehe 27.04.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa