• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

BAJETI YA MANISPAA YATATHMINIWA NA MKUU WA MKOA NA SEKRETARIETI YAKE

Posted on: February 9th, 2024

Mapema mwanzoni wa juma hili, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, mheshimiwa Adam Malima pamoja na sekretarieti yake walifanya kikao cha kwanza cha mapitio ya mpango na bajeti ya Halmashauri ya Manispaa Morogoro kwa kipindi cha miaka mitatu ya fedha, tangu 2020/2021 hadi 2023/2024, na mpango wa bajeti wa mwaka wa fedha 2024/2025.

Kikao hicho kilichofanyika kwa siku mbili kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro na kuhudhuriwa na wataalamu wa Manispaa (CMT) pamoja na mkurugenzi wake, lengo lake lilikuwa ni kutathmini uhai wa Halmashauri kupitia utekelezaji wa shughuli zake za maendeleo, ili kuhakikisha Manispaa inakuwa na mipango yenye ufanisi, na inayojibu changamoto za wananchi.

Katika kikao hicho, menejimenti ya Manispaa ya Morogoro iliwasilisha mapato na matumizi yake, fedha zilizopelekwa kwenye utekelezaji wa miradi ya maendeleo, vijana wanawake na watu wenye ulemavu, taulo za kike, chanjo, na chakula shuleni, kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia 2020/2021 hadi 2023/2024.

Pia menejimenti hiyo iliwasilisha mpango wa bajeti ya Manispaa wa mwaka wa fedha 2024/2025.

Kisha Mkuu wa Mkoa, mheshimiwa Adam Malima akasema ujenzi wa milimani na mafuriko ni miongoni mwa mambo yanayohafifisha jitiada za Manispaa kuwa Jiji hivyo mambo hayo yanapaswa kushughulikiwa kwa weledi na ufanisi hatimaye Manispaa iweze kukidhi vigezo na kuwa jiji.

Naye Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Dkt. Mussa Ali Mussa akaiagiza Manispaa kuwekeza zaidi kwenye maeneo ya milimani kwa kupanda mazao ya kimakakati kama vile karafuu, ili baada ya miaka mitano Halmashauri iweze kuanza kunufaika na uwekezaji huo.

“Cha msingi hapa tusijaribu, tuwekeze kikweli kweli kwa ‘target’ ili baada ya miaka mitano huko mbele basi tuwe tunapata kitu kinachotambulika” alieleza Dtk Mussa.

Kikao cha tathmini ya hali za Halmashauri kimefanyika kwa Halmashauri zote tisa za mkoa wa Morogoro tangu tarehe 31.01.2023 hadi tarehe 05.02.2024.

MWISHO

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa