• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Baruapepe za Watumishi |
    • Malalamiko |
Morogoro Municipal Council
Morogoro Municipal Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
    • Wakuu wa Divisheni na Watumishi
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Divisheni
      • Rasilimaliwatu na Utawala
      • Miundombinu, Uendelezaji wa Vijijini na Mijini
      • Elimu Sekondari
      • Elimu Msingi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Afya, Ustawi wa Jamii na Huduma za Lishe
      • Mipango na Uratibu
    • Vitengo
      • Huduma za Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ugavi na Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi wa Mazingira
      • Fedha na Uhasibu
      • Taka Ngumu na Usafishaji
      • Michezo, Sanaa na Utamaduni
      • TEHAMA
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Elimu
    • Afya
    • Mazingira
    • Miundombinu
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao Vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Meya/Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Iliyoisha
    • Miradi inayoendelea
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Sheria Ndogo
    • Fomu ya Maombi
    • Waraka
    • Hotuba
    • Taarifa kwa Umma
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Picha
  • Market
    • Market line 1
    • Maket line 2

MBIO ZA MWENGE WA UHURU MANISPAA YA MOROGORO

Posted on: April 29th, 2024

Tarehe 28.04. 2024 asubuhi, Mkuu wa Wilaya ya Morogoro mheshimiwa Rebecca Nsemwa, alipokea kutoka kwa Mkuu wa Wilaya ya Kilombero mheshimiwa Dastan Kyoba, Mwenge wa Uhuru pamoja na wakimbizaji wake wa kimkoa na kitaifa.

Mara baada ya kuuopokea Mwenge wa Uhuru, mheshimiwa Nsemwa alitoa salamu za ukaribisho ambapo alieleza kwamba katika Wilaya ya Morogoro, Mwenge wa Uhuru utakimbizwa umbali wa kilomita 216 ukitembelea miradi 18 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi bilioni 6.6.

Mheshimiwa Nsemwa pia amemshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuiletea Wilaya ya Morogoro fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ambayo kwa kweli imesogeza huduma bora kwa wananchi wa Morogoro.

Kwa upande wake Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa (2024) ndugu Godfrey Eliakim Mnzava, amesema agenda kuu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu ni kuhusu utunzaji wa mazingira na uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Mnzava amesema Mwenge wa Uhuru unawaagiza wale wote wanaotaka kuwania uongozi wa Serikali za Mitaa kama wenyeviti wa serikali za mitaa, vijiji, vitongoji, wajumbe wa kamati za mitaa na wa Halmashauri Kuu za vijiji na vitongoji wachukue fomu kwenye vyama vyao vya siasa na fomu ya Serikali ili kupata ridhaa ya kugombea.

Kwa upande wa wananchi, Mnzava amesema Mwenge wa Uhuru unasisitiza kwamba ifikapo wakati wa kampeni wananchi wajitokeze kufika kwenye viwanja vya kampeni ili kuhakikisha wanasikia sera, mipango, maono na mawazo ya wagombea ili wakati wa kuchagua wachague viongozi kutokana na sera na mipango ya viongozi hao.


Vilevile, Mnzava amewataka wananchi wadumishe amani, utlivu na usalama katika maeneo yao wakati wa kipindi chote cha uchaguzi.

Kuhusu utunzaji wa mazingira, Mnzava amesema uchafuzi na uharibifu wa mazingira unaotokana na watu kukata miti hovyo, kuchoma misitu na mapori, shughuli za kilimo zisizozingatia uendelevu na uhifadhi wa mazingira, uchimbaji wa madini, ufugaji wa mifugo mingi bila kuzingatia nyanda za mailisho, na shughuli za viwanda zisizo zingatia uhifadhi wa mazingira, ndio sababu za kuwepo kwa ukame, joto, ardhi kupoteza rutuba, mafuriko na maporomoko.

Mnzava amewataka viongozi na wananchi kushirikiana kwa nguvu kabisa kuhakikisha kwamba wanaendelea kuhifadhi mazingira kwa kuendelea kupanda miti, kuhifadhi na kutunza mazingira ili mazingira nayo yawatunze.

Aidha, Mnzava amepongeza Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Morogoro kwa kufanya manunuzi yote kupitia mfumo wa NeST kisha akaagiza Taasisi zote za Serikali zihakikishe manunuzi yote ya umma yanafanyika kupitia mfumo huo ili kudhibiti ubadhilifu wa fedha za Serikali.

Miongoni mwa miradi iliyotembelwa na Mwenge wa Uhuru katika Manispaa ya Morogoro ni mradi wa ujenzi wa Zahanati ya Kauzeni kwenye kata ya Kauzeni, mradi wa miti wa Mindu kata ya Mindu, ujenzi wa barabara ya kiwango cha zege, ya Kichangani kata Kichangani, ujenzi wa shule ya msingi Viwandani kata Mafisa na ujenzi wa jengo la utawala shule ya sekondari Mkundi kata Mkundi.

MWISHO

 

 

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI February 19, 2025
  • FURSA YA UWEKEZAJI KWA NJIA YA UBIA(PPP) February 18, 2025
  • ZABUNI YA UPANGISHAJI ENEO LA ROCK GARDEN MANISPAA YA MOROGORO August 16, 2022
  • MAPOKEZI YA HELA ZA OC KWA MWEZI JULAI 2022 KIASI CHA TSH 8,714,000.00 August 10, 2022
  • Angalia Yote

Habari Mpya

  • BARAZA LA MADIWANI NA WATUMISHI MANISPAA YA MOROGORO WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HALMASHAURI YA JIJI TANGA

    April 26, 2025
  • KAMATI YA KUDHIBITI UKIMWI MANISPAA YA MOROGORO YATAKA KASI VITA DHIDI YA MAAMBUKIZI MAPYA.

    April 17, 2025
  • KAMATI YA HUDUMA ZA UCHUMI, AFYA NA ELIMU MANISPAA YA MOROGORO YARIDHISHWA NA KASI YA MIRADI YA MAENDELEO.

    April 15, 2025
  • MWENGE WA UHURU KITAIFA WAZINDUA MIRADI YA MAENDELEO YENYE THAMANI ZAIDI YA BILIONI 1.8.

    April 12, 2025
  • Angalia Yote

Video

MEYA KIHANGA AKABIDHI TAULO ZA KIKE KWA WANAFUNZI ZAIDI YA 1600 WA SHULE ZA MSINGI NA SEKONDARI
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu Leseni za Biashara
  • Sheria Ndogo za Manispaa ya Morogoro
  • Sisi ni Nani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Morogoro Modern Market system (outside)
  • Tovuti ya Utumishi
  • Morogoro Modern Market System (LAN Network)
  • Tovuti Rasmi ya Ikulu
  • Tovuti ya RAS Morogoro

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro

    Anuani: 166 morogoro

    Simu: 0232614727

    Simu: 0734-039300

    Baruapepe : info@morogoromc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya Mara kwa Mara
    • Ramani
    • Huduma Zetu

Hatimiliki ©2017 Halmashauri ya Manisaa ya Morogoro. Haki zote zimehifadhiwa